TAASISI YA MANJANO FOUNDATION WAENDELEA KUWANUFAISHA WANAWAKE
![](https://mmi111.whatsapp.net/d/uT3ZLf1yuF7Z0CbS62U2Z1YX8mM/AqPJxU2e7NR9qq4BW6b20jBsg3Jr_Y0NXnGA2xODkSfs.jpg)
![](https://mmi446.whatsapp.net/d/a2bqAfT7IkDLbJF_RF7QgVYX8mQ/AnKqeu4byymURDRrtu4tbnJ46BoDORm6m82PQ0sYLxYa.jpg)
Mafunzo haya yamegawanywa katika awamu mbili ili kumsaidia mjasiriamali wa kike kujikwamua. Awamu ya kwanza ni kumfundisha maswala ya Biashara namna ya kuibua na kubuni miradi mbalimbali namna ya kuandika Mpangilio wa Biashara ikiwemo Matumizi sahihi ya Rasilimali Muda, Fedha, Muda na pia namna ya kujitunzia akiba itokanayo na Biashara yake
![](https://mmi413.whatsapp.net/d/jNOsbv2YhiYFX-3vCm7wtVYX8mw/Aj0PlWwh0f5fWztJ76y2Vb_S3JwP5qRAumK80R9GglUV.jpg)
Awamu ya Pili mshiriki anafundishwa Matumizi sahihi ya Vipodozi kuendana na wakati, mfano office makeup, day, evening na namna ya kumpamba bi Harusi. Pia wanafundishwa namna bora ya kutumia Vipodozi vya LuvTouch Manjano kwa lengo ya kuwa kila mshiriki atakayehitimu mafunzo haya aweze kujiajiri na kujitegemea kwa kuendesha maisha yake ya kila siku kwa kuwapambamba watu wenye Shuguli Mbalimbali kama vile fashion, sendoff, harusi nakadhalika
![](https://mmi445.whatsapp.net/d/T_ifUmU2U35b7Cfo5OMS31YX8m0/Auq3AXXX4O_OKSHHR47kR-qGVAhsW8iaQgbXyNHZzNYp.jpg)
Baada ya Wanawake hawa kuhitimu Mafunzo haya Taasisi ya Manjano Foundation inatoa Mikopo kwajili ya kuwawezesha Kuanzisha Biashara wakiwa chini ya Uangalizi Maalum wa taasisi hiyo kwa Lengo la Kuhakikisha kila Mhitimu wa Mafunzo haya anapiga hatua na kuweza Kujitegemea
0 comments: