MRADI WA KUKWAWEZESHA WANAWAKE WAJASIRIAMALI UNAOFADHILIWA NA TAASISI YA MANJANO WAINGIA MBEYA

Mradi wa Kuwawezesha wanawake Kiuchumi Kupitia Tasnia ya urembo ujulikanao kama Manjano Dream-Makers ulioasisiwa na Taasisi ya Manjano Foundation wataendesha mafunzo ya ujasiriamali kwa wanawake wa Mkoa wa Mbeya kuanzia Jumatatu, tarehe 8 March 2017 kwenye ukumbi wa SIDO Mkoani Mbeya. Mafunzo hayo yatatolewa kwa jumla ya wanawake watakaochaguliwa 30 kutoka mkoani Mbeya. 
Baada ya mafunzo hayo wanaweke hao watakuwa chini ya uangalizi wa Taasisi hiyo kwa lengo la kuhakikisha wanawake wa Mkoa wa Mbeya wanafikia malengo yao waliojiwekea katika kujikita kwenye kujiajiri. Wanawake wakazi wa Mkoa wa Mbeya waliotuma maombi kupitia tovuti ya Manjano Foundation na wanaopenda kunufaika na mradi huo wanaombwa kujitokeza kwa ajili ya usaili siku ya Jumatatu tarehe 6 Machi 2017 kuanzia saa tatu (9:00AM) asubuhi kwenye ukumbi wa wa SIDO Mkoani Mbeya.
Mafunzo yana lengo la kumsaidia mjasiriamali mwanamke kujikwamua na kujiongezea kipato. Awamu ya kwanza ni kumfundisha maswala ya biashara namna ya kuibua na kubuni miradi mbalimbali namna ya kuandika mpangilio wa biashara ikiwemo matumizi sahihi ya rasilimali muda, kutokufuja fedha na pia namna ya kujitunzia akiba itokanayo na biashara yake. 
Awamu ya pili itahusu kuwafundisha jinsi ya kupamba ma harusi na matumizi sahihi ya vipodozi vya LuvTouch Manjano. Baada yanawake hawa kuhitimu mafunzo haya Taasisi ya Manjano Foundation itawaunganisha na taasisi za fedha zinazotoa mikopo bila riba waweze kupata mtaji wa kununua bidhaa za vipodozi kwa ajili ya kuwawezesha kuanzisha biashara wakiwa chini ya uangalizi maalum wa Taasisi hiyo kwa lengo la kuhakikisha kila mhitimu wa mafunzo haya anapiga hatua na kuweza kujitegemea.
Wasiliana nasi kwa Simu namba +255 658 741711 au +255 712 378516


TAASISI YA MANJANO FOUNDATION WAHITIMISHA MAFUNZO YA UJASIRIAMALI MKOA WA DAR ES SALAAM

Afisa Mtendaji Mkuu wa Shear Illusions Africa na Mkurugenzi wa Taasisi ya Manjano Foundation Mama Shekha Nasser akieleza Matumizi Sahihi ya Vipodozi vya Luv Touch Manjano Kwenye Semina ya Ujasiriamali kwa Wanawake wa Mkoa wa Dar es Salaam.Mafunzo ya Ujasiriamali Awamu ya kwa Katika Msimu wa Pili wa Mradi wa Taasisi ya Manjano Foundation ya Mafunzo ya Ujarisiamali kwa wanawake 32 kutoka Mkoa wa Dar es Salaam Yamemalizika. Wanawake 32 wa mkoa wa Dar es salaam ni miongoni mwa wanawake walionufaika na mafunzo ya ujasiriamali na namna ya kupamba kupitia vipodozi vya LuvTouch Manjano. Mafunzo hayo yaliendeshwa na wataalamu wa mambo ya Biashara wakishirikiana na maofisa wa Taasisi ya Manjano. Mafunzo hayo yalilenga kumwezesha mwanamke wa Kitanzania kuondokana na tatizo la ukosefu wa ajira kwa kujikita katika kujiajiri ndani ya Tasnia ya Urembo na vipodozi. Mafunzo hayo yatafanyika kwenye mikoa ya Dar es Salaam, Mbeya,Mtwara,Tabora na Kigoma.Image may contain: 12 people, people sitting and outdoor

Baada yanawake hawa kuhitimu mafunzo haya Taasisi ya Manjano Foundation itawaunganisha na Taasisi za Fedha zinazotoa mikopo bila riba waweze kupata mtaji wa kununua bidhaa za vipodozi kwa ajili ya kuwawezesha kuanzisha biashara wakiwa chini ya uangalizi maalum wa 
Taasisi hiyo kwa lengo la kuhakikisha kila mhitimu wa mafunzo haya anapiga hatua na kuweza kujitegemea.
Washiriki walionufaika kwenye Mafunzo hayo wakiwa katika Picha ya Pamoja na Afisa Mtendaji Mkuu wa Shear Illusions Africa na Mkurugenzi wa Taasisi ya Manjano Foundation Mama Shekha Nasser.Wanawake wa mji wa Dar es Salaam walionufaiki na mafunzo ya ujasiriamali na urembo wamemshukuru Afisa Mtendaji Mkuu wa Shear illusions na Mkurugenzi wa Taasisi ya Manjano Foundation kwa moyo wa kujitolea na kuwajali wanawake wengine hususani wakazi wa Dar es Salaam .
Image may contain: 8 people, people smiling, people standing and sunglasses
Wakiongea zaidi wanawake hao ambao wamepatiwa elimu ya biashara kutambua nafasi yao katika jamii inayowazunguka pamoja na namba ya kupamba maharusi na matumizi ya vipodozi. Wamemshukuru mama Shekha Nasser kwa moyo wenye kuwajali na kuwabeba wanawake wenzake na kutoa elimu ya bure aliyokuwa nayo kwa wengine ili waweze nao kujiongezea kipato na kupunguza ukali wa maisha. Wamemshukuru na wameahidi kuyatumia mafunzo hayo kwa lengo la kujikwamua na tatizo la ukosefu wa ajira kwa wanawake na pia kujiongezea kipato.

JEMIMA SAYS NEVER GIVE UP ON YOUR DREAMS: CELEBRATING BEAUTY, MAKEUP AND SELF-WORTH.

Jemima Joshua was born in Dodoma and grew up in Kagera where she completed her early years of schooling. With a determined personality, Jemima attended University at the Tanzania Research and Career Development Institute (TRACDI) in Dodoma where she studied a degree in Community Development.  
What does your typical day look like?
When I wake up in the morning, the very first thing I do is pray and thank God for protecting me the whole night. After that, I do a little exercise before I eat my breakfast and complete the day’s work.
What does beauty mean to you?
Beauty is something that makes someone look good. It doesn’t matter if you are young or old; everyone has his or her own beauty!
If you were given a chance to use LuvTouch Manjano products, which ones would you use and why?
I would definitely choose the LuvTouch Manjano Foundation if I were given a chance to use their products. I like the foundation because it looks nice and you only need a little at a time. With LuvTouch Manjano’s foundation a little really goes a long way. I also like their foundation because it doesn’t change the color of my skin or make me look pale. Which is different from many foundations in the market.
What Advice do you have for girls and young women?
To my fellow young girls and women, especially those who feel like giving up, my advice to them would be to never give up. Nothing happens by chance. You have to work hard! There are many opportunities if you look for them. You can get funding, grants, scholarships and many things. If you can’t seem to find employment, find something that you are interested or like to do. Maybe you are interested in the hair, beauty and cosmetics industry, or you would like to start a business, then do those things. Giving up is not an option. Also, don’t be afraid to start small. When you start small, you have room to grow and at the end of the day you can be very successful.

AWAMU YA PILI YA MAFUNZO YA WAJASILIAMALI WANAWAKE WA MKOA WA DAR ES SALAAM YALIO CHINI YA TAASISI YA MANJANO YAENDELEA

Mkufunzi wa Maswala ya Biashara Ndugu Felix Maganjila Akitoa Mada kwenye Mradi wa kuwejengea Uwezo wanawake Kwenye Ujasiriamali kupitia Taasisi ya Manjano Foundation. Mafunzo hayo yalianza wiki iliyopita kwa lengo la kuwajengea Uwezo wanwake wa Kitanzania kupitia bidhaa za vipodozi vya LuvTouch Manjano. Washiriki wataweza kujisimamia na kujikita vizuri kwenye biashara ya vipodozi na kujua mbinu mbalimbali za biashara kwa lengo la kumjengea uwezo mwanamke wa Kitanzania.
Image may contain: 3 people, people sitting and text
Washiriki wa Mafunzo ya Usajiriliamali na Urembo yalio chini ya Manjano Foundation wakisiliza kwa makini mada mbalimbali kuhusu mafunzo hayo ya kuwapa uwezo wa kuthubutu kufanya biashara, kujisimamia na kujua mbinu mbalimbali za biashara.Image may contain: 5 people, people standing
Mkurugenzi wa Taasisi ya Manjano Foundation Mama Shekha Nasser Akiwa Katika Picha ya Pamoja na Baadhi ya Washiriki walionufaika na Mradi huo.
Taasisi ya Manjano Foundation, ambayo imeanzisha jukwaa kwa ajili ya kuandaa miradi na programu ambazo zitamuinua mwanamke wa Kitanzania kwa kumwondolea umasikini wa kipato na ambayo itakuwa ni chachu ya kubadili uwezo wake ikiwa pamoja na kuisaidia jamii yake iliyomzunguka. Taasisi hii limekwishazindua mradi wenye kubeba bendera yake, Manjano Dream-Makers, mradi unaokusudia kuzaa kizazi kipya cha wajasiriamali wanawake kwa kutumia kipodozi cha LuvTouch Manjano.

Awamu ya Pili ya Mradi huu Ulizinduliwa na waziri wa Viwanda na Biashara Mh. Charles Mwijage mnamo tarehe 14 Februari 2017, ambapo alisema amefurahishwa sana wwa mwanamke wa Kitanzania kuzindua mradi unaowawezesha wanawake kujiongezea kipato na kujiajiri hasa kwenye sekta ndogo ya Urembo yenye fursa kubwa ya kukua.

SARAH SAYS REMEMBER THAT TOMORROW IS A NEW DAY!: CELEBRATING BEAUTY, MAKEUP AND SELF-WORTH

Sarah Clementina is a young and enthusiastic Masaai lady from Arusha. Born and raised in Arusha, Clementina started her academic career at Green Acres Primary School and worked her way to Kimochi Girls Secondary School for her A-Levels before completing her O-Levels at St. Theresa of the Child Jesus Secondary School. Clementina is currently pursuing her Bachelor’s Degree in Banking and Finance at The Institute of Finance Management.

What does beauty mean to you?
Beauty is an instant attraction! If we are to go by the saying, "beauty is in the eyes of the beholder," then we can wonder why some are considered beautiful and others ugly. So to me beauty is what you instantly see as attractive and appealing to your eyes.

If you were given a chance to use LuvTouch Manjano products, which one would you use and why?
If I were given a chance to use LuvTouch Manjano products, I would choose the powder. The powder is like a 2-in-1 product for me. I like to use it as both a powder and a foundation. I apply it dry with a makeup sponge and it gives medium coverage with a matte finish. It layers well so it can also be used with a wet sponge for fuller coverage. It doesn't make my skin break out and isn't irritating.

What advice do you have for girls and young women?
Do not give up. Anybody can just give up! Whether it is an elderly person, a young person or even a child. Wanting to give up is a normal feeling, just feel that moment and endure it. When you feel like giving up, you may even feel depressed. But, there’s tomorrow. People have to realize and know that whatever it is their feeling for the moment or whatever is happening in their life it doesn’t last forever. That moment will pass. It may hurt, but after a while, the pain diminishes. So, my advice is if you want to give up about something, just remember that that moment will pass. For instance, if you wanted something and you never got it, maybe you’re going to get something even better! Perhaps you wanted something good, but maybe what is coming is the best. So, you wanted something good, you didn’t get it and now you want to give up? That’s not the right thing to do. Just pick up yourself and remember that tomorrow is a new day! Whatever you want can be achieved in many different ways, giving up is not a solution.    

WAZIRI MWIJAGE AZINDUA AWAMU YA PILI YA MAFUNZO YA WAJASILIAMANI WASICHANA YA TAASISI YA MANJANO

Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji ,Charles Mwijage amewataka watanzania kuwekeza katika mfumo unaoweza kutoa ajira za moja kwa moja kwa vijana kama ilivyo katika kampuni ya Manjano Foundation.
Mwijage amesema hayo mapema leo jijini Dar es Salaam alipokuwa akifungua mafunzo ya wanafunzi 30 juu ya masuala ya urembo yanayoendeshwa ta tasisi ya Manjano Foundation ya hapa hapa nchini.

“huyu ni moja ya wawekezaji ambao wanapaswa kuungwa mkono na kila mmoja kwani ameamua kuwekeza kwa kutengeneza bidhaa ambazo zinatumia malighafi kutoka hapa hapa nchini na kuamua kuwawezesha wanawake wadogo kupata mafunzo hili waweze kuingiza pesa kupitia bidhaa hizo” amesema Waziri Mwijage.

Mwijage ameongeza kuwa mbali na Manjano foundation kutoa elimu ya ujasiliamali kwa wasichana hao pia ipo katika mpango kabambe wa kujenga kiwanda mjini kibaha ambapo tayari wameshapata ekeri tatu kwa ajili yakujenga Godown ambalo litasaidia kufanya uzalishaji.

Kwa upande wake mkurugenzi wa Manjano Foundation Shekha Nasser amesema kuwa wasichana ambao wanapata mafunzo kutoka tasisi hiyo wanaweza kuingiza kiasi cha Milioni mbili mpaka tatu kwa mwezi.

Aidha ametaja kuwa program hiyo katika mwaka hu itaweza kuwafikia wanawake katika mikoa mitano nchini hili waweze kujikwamua kiuchumi.
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mh. Charles Mwijage  akipokelewa na Mwasisi wa Taasisi ya Manjano na Mmiliki wa Shear Illusions, Shekha Nasser mara baada ya kuwasili kwa ajili ya ufunguzi wa mafunzo kwa wanawake ikiwa ni awamu ya pili.
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mh. Charles Mwijage akipata maelezo kutoka kwa Mwasisi wa Taasisi ya Manjano na Mmiliki wa Shear Illusions, Shekha Nasser  kuhusu darasa linalotumika katika ufundishaji wa wasichana hao leo katika ofisi ya Shear Illusion iliyopo jengo la Millenium Tower jijini Dar
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mh. Charles Mwijage akizungumza na wanafunzi wa Manjano Academic mara baada ya kufika na kujionea mafunzo hayo leo katika ofisi ya Shear Illusion jijini Dar
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mh. Charles Mwijage akizungumza wakati wa uzinduzi wa programu ya kuwawezesha wanawake kiuchumi ijulikanayo kama "Manjano Dream Makers" kwa awamu ya pili iliyozinduliwa leo na waziri huyo katika ukumbi wa LAPF Millenium Towers jijini Dar es Salaam leo.
Mwasisi wa Taasisi ya Manjano na Mmiliki wa Shear Illusions, Shekha Nasser akizungumza kuhusu uzinduzi rasmi wa program ya ajira kupitia tasnia ndogo ya urembo pamoja na kufanya utambulisho kwa wageni waalikwa.
Afisa Kutoka TFDA Bi. Grace Shimwela akizungumzia umuhimu wa kupata vibali vya urembo "Cosmetics and Personal Care" kwa wanawake walioko na ambao wamemaliza progamu mbalimbali za mafunzo kutoka kwa Manjano Dream Maker ili kuwasaidia pale wanapoanza kujitegemea
Jokate Mwegelo akizungumza jambo kwenye ufunguzi huo
Mshiriki mmoja aliyenufaika na Taasisi ya Manjano, Josephine Rwetela akizungumzia umuhimu wa kutengeneza ajira kupitia Tasnia ndogo ya Urembo nchini.
Mkurugenzi wa GS1 Tanzania, Fatma Khange akitoa maneno ya shukrani kwa wageni waalikwa pamoja na wanawake wanaoshiri kwenye mafunzo hayo yaliyoziduliwa leo na Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mh. Charles Mwijage.
Baadhi ya washiriki walioudhuria katika uzinduzi huo
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mh. Charles Mwijage akimkabidhi cheti Mkurugenzi Mtendaji 8020 Fashion na Mentor wa Taasisi ya Manjano Foundation, Shamim Mwasha
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mh. Charles Mwijage akimkabidhi cheni Mentor wa Taasisi ya Manjano Foundation, Mboni Masimba
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mh. Charles Mwijage  akimkabidhi cheti Mentor wa Taasisi ya Manjano Foundation, Mariam Marion Ndaba
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mh. Charles Mwijage  akiwa kwenye picha ya pamoja na Manjano Academic
Mgeni rasmi Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mh. Charles Mwijage akiwa kwenye picha ya pamoja na Mentor wa Taasisi ya Manjano Foundation.
Mgeni rasmi Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mh. Charles Mwijage akiwa kwenye picha ya pamoja na Dream Makers.

WAZIRI MWIJAGE KUZINDUA AWAMU YA PILI YA MAFUNZO YA WAJASILIAMANI WASICHANA YA TAASISI YA MANJANO

Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage anataraji kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa mafunzo ya wajasiliamli wasichana ya Taasisi ya Manjano, jijini Dar es Salaam.Shear Illusion kupitia bidhaa yake ya manjano imeanzisha mpango maalum wa kusaidia kutoa ajira kwa wanawake ambao wamemaliza shule na kushindwa kupata kazi.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, afisa mtendaji mkuu wa Taasisi ya Manjano na Kampuni ya Shear Illusions Ltd, Shekha Nasser amesema ameamua kumualika Waziri Mwijage ili aweze kuona fursa zilizopo katika viwanda vidogo vidogo 
Amesema kuwa mara baada ya kuona tatizo hilo wakaamua kuanzisha mradi wa uuzaji wa bidhaa za manjano kwa wanawake mbalimbali waliopo jijini Dar ese Salaam na mikoa mingine.
“tasnia hii ya urembo ni moja ya vitu vinavyoweza kumsaidia mwanamke kuingiza zaidi ya shilingi milioni mbili kwa mwezi kama mtu atakuwa mwaminifu na biashara na kuifanya hii kuwa ni kazi yake ya muhimu katika kujikwamua kiuchumi” amesema. Shekha Nasser
Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Manjano na Shear Illusion LTD, Shekha Nasser akizungumza na waandishi wa habari wakati kutangaza uzinduzi wa awamu ya pili ya mafunzo ya wajasiliamli wasichana ya Taasisi ya Manjano, Jijini Dar es salaam leo.Amesema kuwa katika kuhakikisha kuwa wanatoa ajira kwa wasichana hao wameamua kutoamafunzo ya wiki mbili kwa wasichana 30 ambao watapewa mtaji wa shilingi 300,000/-Amesema kuwa wasichana hao ambao wapo 30 wamepatikana kutokana na mchujo uliofanywa na watalaamu wa masuala ya urembo hadi kufikia hapo.
Sehemu ya Washiriki waliofuzu kujiunga na mafunzo ya wajasiliamli wasichana ya Taasisi ya Manjano.